Wananchi wakisubiri daladala bila matumaini yoyote kufuatia mgomo asubuhi hii, Mwang'ingo, Manispaa ya Iringa
MGOMO wa daladala katika Manispaa ya Iringa umeanza asubuhi hii katika eneo la Mwang'ingo, kwa madereva na wamiliki wa daladala kudai kuchoshwa na manyanyaso ya SUMATRA mkoa wa Iringa.
Mgomo huo umekuja kutokana na kuchukizwa uamuzi wa Sumatra mkoa wa Iringa kufuta stendi ya posta pamoja na kuzuia daladala kukaa kwa muda eneo la stendi ya daladala ya Miyomboni.