Jumuiya ya Uamsho na Mihadhara ya
Kislamu (JUMIKI) imekusanya zaidi ya majina elfu 60 na saini zao kwa
ajili ya kudai kura ya maoni ya kukataa au kuukubali Muungano.
Akitoa taarifa ya Jumuiya hiyo kwa
wandishi wa habari huko hoteli ya Mazson, Naibu Amir wa Uamsho, Sheikh
Haji Ali amesema jumuiya hiyo inaamini Muungano uliopo umefanywa bila ya
ridhaa ya wananchi.
Amesema hivi sasa umefika wakati kwa Wanzanzibari kudai kura ya maoni na mustakabali wa Zanzibar.
Aidha, Sheikh Ali amesema Uamsho itaendelea na shughuli zake za kuelimisha, kutetea na kudai Zanzibar yenye
mamlaka kamili Kitaifa na Kimataifa bila ya kuvunja sheria na taratibu za nchi.
Amesema baadhi ya viongozi kwa utashi
wao wa kisiasa wamejaribu kuzuia mihadhara ya Jumuiya hiyo, lakini
hatua hiyo imefanyika nje ya sheria kwa vile Jumuiya hiyo imesajiliwa
kisheria.
Wakati huo huo, jumuiya hiyo
imekanusha taarifa zainazoenezwa na vyombo vya habari na wanasiasa
kuihusha na vurugu na vitendo vya uvunjifu wa amani ikiwemo uchomaji wa
makanisa, maskani na mauaji.