Search in This Blog

M to the P BADO YUPO HAI


Albert Mangwea 'Ngwair' na M to the P
Kumekuwepo na sintofahamu kuhusu hali ya msanii M To The P ambae alikuwa rafiki wa karibu wa marehemu Albert Mangwea a.k.a Ngwair, msanii huyu inasemekana alikuwa na marehemu wakitumia pombe kali na madawa ya kulevya na kujikuta wanazima wote katika chumba kimoja na kukimbizwa St.Hellen Hospital ambapo umauti ulimfika Ngwair. 

Kwa kuwa ripoti zinapatikana kutoka Afrika kusini na wachache sana ndio wenye mawasiliano ya moja kwa moja na watu walioko hospitalini hapo na hadi sasa hakuna mzungumzaji maalum aliyeteuliwa kutoa taarifa kutoka hospitalini hapo, inaweza kuwa chanzo cha habari kutofautiana.

Kwa waliosikiliza TBC Taifa saa kumi katika kipindi cha ‘harakati’ wametangaza kuwa M to the P amefariki dunia asubuhi ya leo na mipango ya kusafirisha miili ya wawili hao inaendelea.

Lakini habari za uhakika zilizopatikana ni kwamba msanii huyo bado yuko hai japokuwa hali yake ni mbaya sana.

Msanii Bushoke na baadhi ya ndugu wa marehemu tayari wako Afrika kusini na ripoti zilizopatikana kutoka kwao zinasema msanii M to the P anaendelea vizuri, japo alikuwa anapumulia mashine alipowaona alipata nguvu akanyanyuka kidogo akiwa pale pale kitandani.

Millard Ayo mtangazaji wa kipindi cha amplifaya cha Clouds Fm ambae yuko katika hospitali ya St. Hellen Johannesburg, amethibisha kuwa M to the P yuko hai. Hii ni tweet yake muda mfupi uliopita.


“#BREAKING Sio kweli kwamba m2theP kafariki, ni mzima ila anapumulia mashine, kafungua macho na kunyanyua miguu dakika chache zilizopita.”

Watanzania waliofika hospitalini hapo wamepata nafasi ya kuuangalia mwili wa marehemu na wanasema walikuwa nae hadi jana majira ya saa kumi jioni, inasikitisha sana.

Mipango ya kusafirisha mwili wa marehemu bado inaendelea.
 
Support : KARIBU TENA MDADISI MAM
Copyright © 2011. RISASI - Haki Zote Zimehifadhiwa.
KWA HISANI YA MDADISI MAMBO
Proudly powered by Blogger