Wananchi
wakiangalia mwili wa aliyekuwa Mfanyabiashara wa katika moja ya maduka
ya Kariakoo aliyetambulika kwa jina moja la Shirima, aliyejirusha kutoka
ghorofa ya 9 ya Hoteli ya Concord ni leo mchana huu maeneo ya Kariakoo.
Mashuhuda
wa tukio hilo lililotokea, wameeleza kuwa walipatwa na mshuko mkubwa
baada ya kusikika kishindo cha kitu kilichoangua na kuhisi labda ni
'yale yale' ya maghorofa kuporomoka yenyewe baada ya kuguswa na Kunguru,
kumbe ni mtu huyo aliyeanguja juu gari hilo.
Na
baada ya watu hao kusogea eneo hilo walikuta ni mwili wa mtu
aliyeanguka kutoa ghorofani ambaye baadhi yao waliweza kumtambua kwa
jina moja kuwa ni Shirima. Baada ya tukio hilo wasamaria wema
wamemkimbiza mtu huyo hospitali kutokana na kwamba alikuwa bado akipumua