Kampuni ya uchimbaji madini ya Lonmin, nchini Afrika Kusini inasema kuwa
maelfu ya wafanyakazi katika mgodi wake wa wa platinum wamefanya mgomo
kinyume cha sheria baada ya afisa wa muungano wao kupigwa risasi katika
baa moja mwishioni mwa juma.
Msemaji wa kampuni hiyo Sue Vey amesema kuwa shughuli zote za uzalishaji kwenye kiwanda hicho zimevurugika .
Mwezi Agosti mwaka jana wafanyakazi
thelathini na wanne waliuliwa na polisi katika mgodi wa Marikana na
waandishi wa habari wanasema mgomo huo umesababisha hofu ya kutokea kwa
ghasia kufuatia hali ya taharuki iliyopo juu ya kukatwa kwa kazi ,
mashauriano ya riba na uhasama ndani ya muungano wa wafanyakazi.Mgomo huu umezua hofu ya vurugu zaidi kutokea baada ya sekta hiyo kukumbwa na migomo mwaka jana
Lonmin, ambayo hisa zake,ziko katika soko la hisa la London na
Johannesburg , ndiyo kampuni ya tatu kwa ukubwa katika kuzalisha madini
ya platinum.
Taarifa za mgomo wa leo zimesababisha hisa za kampuni hiyo kushuka kwa asilimia 5% mjini London.
Msemaji wa kampuni hiyo, Sue Vey alisema kuwa migodi yote kumi na mitatu ya kampuni hiyo imefungwa kwa sasa.
"Wafanyakazi wa kampuni hiyo waliwasili kazini ingawa hawakuelekea katika shughuli zao kama ilivyo desturi yao
Huku akisema kuwa kampuni hiyo haielewi kwa nini wafanyakazi wameamua
kugoma, msemaji wa chama cha wafanyakazi hao, alisema kuwa huenda mgomo
huo unatokana na ghadhabu ya wafanyakazi hao, kuhusu mauaji yaliyotokea
mwishoni mwa wiki ya kiongozi mmoja wa chama hasimu cha wafanyakazi.
Polisi walithibitisha kuwa kiongozi huyo aliuawa mwishini mwa wiki katika eneo Rustenburg.