Search in This Blog

AWAMU YA PILI YA MAJINA YA WALIOHITIMU KIDATO CHA SITA NA KAMBI ZA JKT WALIZOPANGIWA...TAREHE YA KURIPOTI NI 24 JUNI MWAKA HUU.

Jeshi la kujenga taifa (jkt) linawatangazia vijana waliomaliza kidato cha sita 2013 na kuchaguliwa kujiunga na jkt katika makambi ya ruvu pwani, mgambo tanga, msange tabora, bulombora kigoma, maramba tanga, rwamkoma mara, mlale ruvuma na kanembwa kigoma kuripoti katika makambi hayo tarehe 24 juni 2013 kama ilivyotangazwa awali.
vijana hao waripoti katika makambi waliyopangiwa kama ilivyoonyesha katika tovuti ya jkt www.jkt.go.tz. atakayeripoti kambi ambayo hakupangiwa hatapokelewa. vijana hao walipoti wakiwa na vyeti vya leaving vya kidato cha nne au cha sita kwa uthibitisho

inasisitizwa kuwa kujiunga na jkt kwa mujibu wa sheria ni lazima, atakayeshindwa kuripoti atakuwa amevunja sheria na atachukuliwa hatua za kisheria

vijana watunze tiketi zao walizotumia kwenda katika makambi ya jkt. nauli zao zitarejeshwa na jkt watakaporipoti kambini.

vijana waliochaguliwa katika awamu ya pili ni wale waliofauru kwa divisioni, ii na baadhi ya division iii mchepuo wa sayansi.

vijana wa kidato cha sita 2013 ambao majina yao hayakuorodheshwa katika tovuti hiyo, watajiunga na jkt awamu ya tatu mwezi septemba 2013




 
Support : KARIBU TENA MDADISI MAM
Copyright © 2011. RISASI - Haki Zote Zimehifadhiwa.
KWA HISANI YA MDADISI MAMBO
Proudly powered by Blogger