Moja ya couple zilizozaliwa katika msimu wa 8 wa Big Brother Africa
‘The Chase’ (2013), ni ya LK4 wa Uganda pamoja na Koketso wa Afrika
Kusini ambao baada ya wote kutolewa mjengoni sasa wanaendelea kustawisha
kile tunachoamini kuwa (love at first sight).
Siku kadhaa zilizopita baada ya LK4 kurudi nchini kwao Uganda
alitweet kuwa kuna ‘Eviction party’ inakuja, na kuongeza kuwa kama
mambo yataenda vizuri anategemea kupata mgeni rasmi japo hakumtaja kwa jina na kutuachia uwanja wa kutabiri kuwa ni kipenzi chake Koketso.
Siku zikaenda bila kupata updates zozote kuhusu party hiyo wala mgeni
huyo mpaka alhamisi iliyopita (June 20) baada ya Koketso kutweet,
“Hello lovelys!!! Flying out won’t be tweeting till tomorrow. Miss you
all already;)”, ndio watu wakahisi huenda ndio safari ya yule mgeni
ambaye LK4 anamtegemea.
Kesho yake Ijumaa (June 21) LK4 aliweka picha ya yeye na Koketso
wakiwa kwenye gari (huenda wakitokea airport baada ya kumpokea mgeni
wake aliyewasili Uganda) iliyosindikizwa na tweet hii, “Life in the
Emerald house is great and amazing! They say love conquers all, even
borders, well, Is it true? Stay tuned.”.
Kutokana na lovebirds hawa kutaka kutwist kidogo akili za followers
wao wa twitter, mrembo kutoka South Africa Koketso naye alitweet tena
Jumamosi (June 22) “Hello Africa! Oook I’m good but don’t ask where I
am. Lol!”
Well, kwasababu wameamua kutoa matukio kwa episodes tutegemee updates
mpya kutoka kwa wawili hawa ambao inaonekana wanampango wa kutu
surprise, lets wait and see!