Kile kipindi maarufu cha TV cha Mkasi ambacho
hurushwa na channel ya EATV, kitaendelea tena season ya pili hivi
karibuni na moja ya watu waliopata bahati ya kuhojiwa ndani ya kipindi
hicho ni mwanadada Jokate mwengelo (Muigizaji na mjasiriamali) katika
season hii mpya.
Bongo movies tulipata nafasi ya kuzungumza na mmoja wa waandaaji wa
kipindi hicho kuweza kupata baadhi ya mawili matatu ambayo mlimbwende
huyo atayazungumzia. Baadhi ya mambo ambayo dada yetu atafunguka kwenye
show hii ni haya yafuatayo.
1. Maendeleo ya kampuni yake ya kidoti toka ilipoanzishwa mpaka sasa
2. Story za maisha yake ya mahusiano na ukweli mzima wa ishu yake na Diamond Platnumz
3. Mipango yake ya baadaye na kampuni yake ya kidoti