Search in This Blog

MHE HALIMA MDEE, WOLPER WAJIFUA KWA NYAKATI TOFAUTI KABLA HAWAJAVAANA KATIKA ULINGONI.


Mdee amekuwa akiendelea na mazoezi yak echini ya Mbunge wa CCM, Idd Azzan ambaye pia siku hiyo atapanda ulingoni kutoana jasho na mkali wa Bongo Movie Jacob Steven ‘JB’

Mbunge wa Kawe (Chandema), Halima Mdee ameanza maandalizi yake ya pambano la ngumi dhidi ya staa wa Bongo Movies, Jacqueline Wolper.
Pambano la wakali hao litafanyika Julai 7, siku ya Sabasaba katika Tamasha la Matumaini kwenye Uwanja we Taifa jijini Dar es Salaam.

Katika tamasha hilo mwaka jana Wolper alionyesha uwezo kuliko Wema Sepetu katika pambano lao lililosisimua.
Lakini Mdee ametamba kumpoteza Wolper katika pambano lao hilo la Julai 7.
Mdee anaendelea na mazoezi mjini Dodoma, wakati Wolper anaendelea na mazoezi jijini Dar es Salaam.
 
Support : KARIBU TENA MDADISI MAM
Copyright © 2011. RISASI - Haki Zote Zimehifadhiwa.
KWA HISANI YA MDADISI MAMBO
Proudly powered by Blogger