Habari hizo zimekuja kupitia taarifa iliyotolewa na ofisi ya rais ya Afrika kusini.Taarifa hiyo imesema kuwa mzee Mandela ameendelea kusalia hospitalini mjini pretoria kwa siku kumi na sita akitibiwa mapafu yaliyo sababisha tatizo kwenye mfumo wake wa upumuaji.
Rais wa Afrika kusini Jacob Zuma amemtembelea mzee mandela jumapili jioni na kuzungumza na jopo la matibabu wanao mtibia.
Baadaye bwana Zuma alilejea kauli yake ya kulitaka taifa na dunia kumuombea mzee Mandela apate nafuu.