Search in This Blog

NEYMAR AANZA VYEMA KOMBE LA MABARA 2013 BRAZIL IKIUA 3-0

Party time: Chelsea star David Luiz gets involved with the celebrations
Nyota wa Chelsea, David Luiz akishangilia na wenzake
MSHAMBULIAJI mpya wa Barcelona,Neymar jana aling'ara katika ufunguzi wa michuano ya Kombe la Mabara, akifunga bao la mapema dakika ya tatu wakati Brazil inailaza 3-0 Japan.
Mshambuliaj huyo nyota wa Brazil, alifunga kwa shuti la nje ya eneo la hatari, akiunganisha pasi ya Fred ambaye naye alipokea krosi ya Marcelo kwa kifua kwanza.
Paulinho alifunga la pili dakika ya 48 kwa pasi ya Dani Alves na Jo akafunga la tatu dakika ya 90.
Ushindi huo unaiweka Brazil kileleni mwa Kundi A kwa pointi zake tatu. Italia na Mexico watamenyana leo katika mechi nyingine ya kundi hilo.
Kikosi cha Brazil jana kilikuwa; Julio Cesar, Dani Alves, Thiago Silva, Luiz, Marcelo, Oscar, Gustavo, Paulinho, Fred/Jo dk81, Neymar/Lucas Moura dk74 na Hulk/Hernanes dk75.
Japan: Kawashima, Konno, Nagatomo, Uchida, Yoshida, Endo/Hosogai dk77, Honda/Inui dk88, Kiyotake/Maeda dk51,Kagawa, Hasebe na Okazaki.
Neymar
Neymar
Chukua hiyo: Neymar aling'ara jana
Neymar's goal
Neymar's goal

 
Support : KARIBU TENA MDADISI MAM
Copyright © 2011. RISASI - Haki Zote Zimehifadhiwa.
KWA HISANI YA MDADISI MAMBO
Proudly powered by Blogger