STEVEN KANUMBA JR AZALIWA, MAMA KANUMBA, MAMA LULU NA LULU WAJAWA NA FURAHA.
Mama Lulu na mama wa marehemu Steven Kanumba wanaonekana kuwa karibu
sana siku hizi na hivyo watu kuzidi kuamini kuwa hawana tofauti tena na
kusahau yaliyopita. Dada wa marehemu Steven Kanumba amejifungua hivi
karibuni katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili na mtoto huyo kupewa
jina la Steven Kanumba Jr huku mama mzazi wa Elizabeth Michael(Lulu) na
mama Kanumba wakiwa na furaha sana, Lulu pia alionyesha furaha yake kwa
kuzaliwa mtoto huyo kama picha zinavyoonekana hapo chini. Tunawapongeza
tena na tena wazazi hao kwa kuwadhihirishia wanajamii kwa mara nyingine
kuwa kila mtu ana amani na mwenzake na hakuna tofauti yoyote kati yao.
Angalia picha...........