Search in This Blog

JWTZ LASUBIRI KIBALI KUTOKA KWA UMOJA WA MATIFA KUJIBU MAPIGO DAFUR NCHINI SUDAN


JESHI la wananchi JWTZ limesema kuwa linasubiri kibali kutoka kwa umoja wa mataifa ili kujibu mapigo kwa waasi waliofanya shambulizi dhidi ya kikosi cha UN na kuua wanajeshi saba watanzania huku wakiwajeruhi wengine kadhaa.

Kanali Kapambale Mgawe alisema endapo wakipewa ruhusu kutoka kwa UN watafanya hivyo lakini kwa sasa hawawezi kutokana na sheria zilizopo.

Aidha kanali mgawe ameongeza na kusema miili ya wanajeshi hao saba hivi sasa inafanyiwa uchunguzi na timu ya wataalamu ya umoja wa mataifa na kisha baada ya hapo italetwa nchini ambapo itahifadhiwa katika hospitali ya lugalo na kisha baadae kupelekwa wizara ya ulinzi kwa ajili ya heshima za mwisho kwa ndugu, jamaa na marafiki.

Ili kubaini chanzo cha kuuwawa kwa askari hao, tayari jeshi la wananchi limeteua timu ya wataalamu ambayo itaelekea Darfur kuchunguza kwa kina mauaji hayo ambayo ni makubwa kutokea kwa askari wanaolinda amani wa umoja wa mataifa.

Umoja wa Mataifa waaswa:
Umoja wa mataifa umetakiwa kuangalia usalama wa wanajeshi wanaolinda amani katika sehemu mbalimbali duniani ili kuzuia wanajeshi hao kuendelea kushambuliwa na hatimaye kuuwawa pindi wanapokuwa kazini.

Kauli hiyo imetolewa na mhadhiri mwandamizi wa sayansi ya siasa na utawala kutoka chuo kikuu cha Dar es Salaam, Dr Lupa Ramadhani wakati akielezea tukio la kuuwawa wanajeshi saba watanzania mjini Darfur nchini Sudan.

Dr Lupa ameutaka umoja wa mataifa kutunga sheria zitakazozidi kuwalinda wanajeshi wanaolinda amani ikiwezekana kulegeza sheria za sasa zinazowazuia wanajeshi kupambana na waasi.

Kuhusianan na mahusiano ya kidiplomasia kati ya tanzaia na sudan kusini, Dr Lupa amesema shambulizi hilo haliwezi kuathiri urafiki uliopo baina ya nchi hizo kwani hata waasi hao hawatambuliwi na serikali ya sudan kusini.
 
Support : KARIBU TENA MDADISI MAM
Copyright © 2011. RISASI - Haki Zote Zimehifadhiwa.
KWA HISANI YA MDADISI MAMBO
Proudly powered by Blogger