Husna Maulid.
Akizungumza na paparazi, Husna alisema amelazimika kukatisha
kufunga baada ya kuugua malaria na kumfanya kuendelea na dozi lakini
hali bado haijawa nzuri kwani mwili wake unakosa nguvu.“Naumia sana kushindwa kuendelea na mfungo kwa sababu ya kuumwa sijui kwa nini malaria inanitesa hivi, lakini nikipona nitalipiza siku ambazo sijafunga kwani mwezi huu ni wa toba na ninamuomba Mungu anitimizie kila ninachokihitaji katika maisha yangu,” alisema Husna.
Hivi karibuni Husna alitundika picha katika mtandao wa Instagram inayomuonesha akiwa mjamzito, alipoulizwa na paparazi wetu juu ya hilo alisema siyo mjamzito.