Mtoto Ashura Mustapha anayesumbuliwa na ugonjwa wa kansa ya ngozi.
MTOTO Ashura Mustapha (7) mkazi
wa Mwandege, wilayani Mkuranga, Pwani anasumbuliwa na ugonjwa wa kansa
ya ngozi tangu akiwa na mwaka mmoja.
Akizungumza na mwandishi wetu, baba mzazi wa mtoto huyo, Mustapha
Makombe alisema: “Mwanangu anateseka sana jamani, ugonjwa ulianza kama
malengelenge akiwa na umri wa mwaka mmoja tukawa tunakwenda hospitali
ndogondogo lakini baadaye tukaamua kumpeleka Muhimbili ambapo tulipewa
barua ya kutuelekeza kwenda CCBRT, kule ndipo wakagundua mwanangu ana
kansa ya ngozi steji ya nne.
“Baada ya kuhangaika katika hospitali
nyingi bila mafanikio, nikaamua kwenda Hospitali ya Regency (Dar) kuomba
msaada wa kwenda kutibiwa India.
“Pale waliniambia nichangie
shilingi milioni moja na laki tano kwa ajili ya tiketi na viza ili
mwanangu akatibiwe India, hizo hela mimi sina. Naomba Watanzania
mnisaidie hata kwa fedha za mitandao kwa namba 0769 517765 na 0715
424697 ili niweze kumpeleka mwanangu India akatibiwe,” alisema baba
mzazi.