Search in This Blog

WAKUU WA GEREZA WATIMULIWA WAKIHUSISHWA NA UJANGILI KITETO MANYARA.

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiEZbmheEWsXOwS9zn4K-Shaq7vUAdsw3OsL5erJuv_LWjzvi9XFzfudVJ82gbwOGyOc-ZP1FrEEVDujY_xc8DgeUiCfV9sJVwERtX6NSaFdAjHGUezoB2kBLvZ4gbtEt_3pL14t35lHw10/s1600/tusks.jpgDAR ES SALAAM.  SERIKALI imewafukuza kazi Mkuu wa Gereza la Kiteto, Mrakibu wa Magereza, Ally Sauko na Msaidizi wake Mrakibu Msaidizi wa Magereza Joseph Kimaro, baada ya kukamatwa na askari wa Kikosi cha Kuzuia Ujangili Kanda ya Kati wakiwa na nyara za Serikali.

Hivi karibuni Jeshi la Magereza lilitoa taarifa kwamba mkuu huyo, amevuliwa uongozi na kuhamishiwa Ofisi ya Mkuu wa Magereza wa Mkoa wa Manyara, akisubiri maamuzi ya mamlaka ya kinidhamu wakati Kimaro alifung uliwa mashtaka na kusimamishwa kazi akisubiri maamuzi ya mamlaka ya kinidhamu.

Maofisa hao ni miongoni mwa askari saba waliokamatwa na kikosi hicho Julai 23 mwaka huu, wakiwa na nyara za Serikali zenye thamani ya Sh55 milioni.

Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Ndani, Isaac Nantanga, aliwaambia waandishi wa habari jana kuwa maofisa hao wamefukuzwa kazi kutokana na matumizi mabaya ya madaraka kwa kuruhusu gari na silaha za Serikali kutumika katika ujangili.

“Matukio ya uhalifu kwa watendaji wa vyombo vya dola yanaleta mshtuko mkubwa kwenye jamii na inaonekana ni suala linaloanza kukua,”alisema Nantanga.

Alisema maofisa wengine wa ngazi za chini waliokamatwa wakiwa na nyara walishafukuzwa kazi na Kamishna wa Magereza Nchini.

Katika hatua nyingine, Msemaji huyo alisema zaidi ya wakimbizi 500,000 wamerejeshwa kwao tangu zoezi hilo lilipoanza mwaka 2002. MWANANCHI.
 
Support : KARIBU TENA MDADISI MAM
Copyright © 2011. RISASI - Haki Zote Zimehifadhiwa.
KWA HISANI YA MDADISI MAMBO
Proudly powered by Blogger