KOCHA
Roberto Mancini leo amekwenda mjini Istanbul, Uturukikufanya mazungumzo
ya kusaini Mkataba wa miaka mitatu kuifundisha Galatasaray utakaokuwa
na thamani ya Pauni Milioni 4.6 kwa mwaka.
Mancini,
amekuwa 'juu ya mawe' tangu atupiwe virago Manchester City mwishoni mwa
msimu na anatarajiwa kutambulishwa kurithi mikoba ya Fatih Terim
Jumanne.
Mabingwa
hao wa Uturuki pia wamekubali kumlipa Mtaliano huyo bonasi ya Pauni
Milioni 5.86 kama watavuka hatua waliyofika mwaka jana Ligi ya Mabingwa
na kufanikiwa kuingia Robo Fainali.
Kimeeleweka: Roberto Mancini yupo Uturuki kukamilisha mazungumzo ya kujiunga na Galatasary
Juu ya mawe noma: Mancini alifukuzwa Manchester City Mei, mwaka huu
Mancini
anatarajiwa kukutana na Rais wa klabu, Unal Aysal Jumatatu kufikia
makubaliano ya mwisho ya Mkataba, kwa mujibu wa wakala Muzzi Ozcan
ambaye alifanikisha kuziunganisha pande hizo mbili, baada ya klabu hiyo
kumfukuza Terim.
Uturuki sasa: Galatasaray inamtaka Mtaliano huyu