Jeshi la Polisi Kanda maalumu ya Dar es Salaam
limewatoa hofu wananchi wanaofanya shughuli zao kwenye maeneo ya mikusanyiko,
kufuatia shambulio lililotokea kwenye maduka ya Westgate, yaliyopo jijini
Nairobi Kenya, na kusababisha vifo vya zaidi ya watu 65 na wengine zaidi ya 170
kujeruhiwa vibaya.
Kamanda Kova
Kamishna
wa Kanda hiyo Suleiman Kova amesema tangu kutokea kwa tukio hilo, jeshi hilo
limeimarisha ulinzi huku wakiwataka wananchi kutoa taarifa za watu wanaowatilia
mashaka (Star TV).
Wakati
huo huko Kenya
Majeshi
ya Kenya yamechukua udhibiti wa mall hiyo ya Westgate iliyoshambuliwa na
wanamgambo wa al-Shabab, na kwa sasa yanafanya operesheni ya mwisho baada ya
mateka wote kuokolewa.
Milipuko
na milio ya risasi imesikika ndani ya mall hiyo leo asubuhi, saa chache baada
ya vikosi vya Kenya kuidhibiti kutoka kwa washambuliaji hao. Takriban watu 62
wameuawa na wengine 200 kujeruhiwa kwenye shambulio hilo la Jumamosi lakini
idadi ya watu waliopoteza maisha inaweza kuongezeka. Watu 63 hawajulikani
walipo.
Kundi
hilo la kigaidi limedai kufanya shambulio kama kisasi dhidi ya operesheni za
jeshi la Kenya nchini Somalia.