Marehemu Julius Nyaisangah
(katikati) akiwa katika pozi na Meneja Mkuu wa Global Publishers
Abdallah Mrisho (kushoto) na Mhariri Msaidizi wa Gazeti la Uwazi Elvan
Stambul (kulia) walipokuwa katika semina ya wanahabari Bagamoyo mwaka
2011.
HABARI
zilizotufikia kutoka mkoani Morogoro ni kwamba Mtangazaji Mkongwe
nchini, Julius Nyaisangah 'Uncle J' ameaga dunia. Mpaka mauti yanamfika,
Marehemu Nyaisangah alikuwa Meneja Mkuu wa Abood Media iliyopo mkoani
Morogoro. Marehemu aliwahi pia kufanya kazi katika kituo cha Redio
Tanzania Dar es Salaam (RTD) na katika Kituo cha Redio One ambapo
alikuwa Mkurugenzi. Mpaka sasa chanzo cha kifo chake bado hakijafahamika
japo marehemu alikuwa akiugua kwa muda mrefu. Mungu ailaze roho ya
marehemu mahali pema peponi. AMEN! Taarifa zaidi zitawajia baadaye.