Zimekuwa ni siku nyingi za
kubashiri kuhusu kilichojiri wakati wakenya walipotekwa nyara na
magaidi kwa siku nne mtawalia.
Wakenya zaidi ya sitini walipoteza maisha yao katika jumba la Westgate lakini
hadi sasa Wakenya hawajajua ukweli kuhusu yaliyojiri katika jumba la Westgate.
- Je ni kweli kuna waliokuwa wametekwa nyara na magaidi na kuzuiliwa
katika jumba hilo?
- Je ni kweli kuna magaidi waliouawa na wanajeshi?
Meza ya upekuzi ya Jicho Pevu na Inside Story usiku na mchana wamekuwa
wakidurusu kila ukurasa na kufanya mahojiano na kupitia hatua kwa hatua video
za CCTV kutoka jumba la Westgate na sasa wako tayari kukusimulia kilichojiri.