Search in This Blog

24 WAFARIKI DUNIA KWENYE AJALI YA TRENI NA BASI NDOGO HUKO MISRI

 Takriban watu 24 wamefariki na wengine 28 kujeruhiwa katika ajali ya treni na basi ndogo iliyohusisha magari mengine Kusini mwa mji mkuu wa Misri Cairo.
Treni iligongana na basi ilipokua inatoka mjini Bani Swaif, na kisha kugonga mahari mengine katika makutano ya njia ya reli umbali wa kilomita 40 kutoka mji mkuu Cairo.
Taarifa za vyombo vya habari nchini humo zilisema kuwa wengi wa waliofariki walikuwa jamaa wa familia moja waliokuwa wanarejea kutoka harusini.
Ajali hiyo ilitokea karibu na kijiji cha Dahshur Jumatatu asubuhi huku taarifa zikisema kuwa ajali hiyo pia ilihusisha basi ndogo na magari mengine.
Maafisa wakuu walisema kuwa milango ya magari kuvukia njia ya reli ilikuwa imefungwa lakini dereva wa treni alishangazwa kuona magari yakipita kwenye njia hiyo.
Magari ya kuwabeba wagonjwa ya Ambulance, yaliwasili katika eneo la tukio kuwabeba waliojeruhiwa.
Taarifa zinasema kuna hofu kuwa idadi ya waliojeruhiwa huenda ikaongezeka.
 
Support : KARIBU TENA MDADISI MAM
Copyright © 2011. RISASI - Haki Zote Zimehifadhiwa.
KWA HISANI YA MDADISI MAMBO
Proudly powered by Blogger