Search in This Blog

MKE WA JIRANI YANGU AMENITUKANA KAMA VILE MIMI NI MTOTO MDOGO

Kuna familia moja imejengea karibu kabisa na kwangu tokea wamehamia ni miezi minne na zaidi, Baba wa familia hii ni wa rika langu kabisa, siku chache baada ya kuhamia tulikutana kwenye Ibada ya Jumuia mtaa wa tatu, basi tukawa tunaongea kwa kutaniana akiniuliza wenyeji huwa mnanywea bia wapi? Mimi nikamshauri kwamba Wikiend tutafutane akiwa anasikia hata mkewe.

From there onward inapotokea mmoja wetu amekaa sehemu anapata kinywaji tunashtuana na kama upo interested una-join au unapotezea na mara nyingi tumekuwa tukikutana baadhi ya Weekends au public holidays.

Majuzi nilikuwa na Business moja ya kumshirikisha, tukakubaliana tuonane Lunch time kwasababu wote tunafanya kazi mjini, Kutokana na mda wa Lunch kuwa tight kidogo tulishindwa kupata mda wa kuzungumza kwani kulikuwa na marafiki wengine ambao isingekuwa vema wasikie mambo yetu, hivyo tukakubaliana tukutane Jioni Bar moja ya karibu mtaani kwetu.

Mida ya saa moja na nusu usiku tukakutana na jamaa na tukaanza mazungumzo, tukiwa kati kati ya mazungumzo jamaa akawa busy sana na simu ya mkononi kwani alikuwa kila baada ya dakika chache ananyanyuka kwenda kuongea na simu alafu akirudi 'mudi' yake inabadirika, sikutaka kumuuliza maana niliamini ni mambo yake binafsi na ndomaana hakutaka nisikie anaongea nini.

Baadaye jamaa akazima simu yake, tukaendelea na mazungumzo huku tukipata Bia mbili tatu, ilipofika saa tatu na dakika kadhaa usiku nikapigiwa simu na namba ambayo sikuwa nimei-save, nikasikia sauti ya mdada lakini siku-notice ni nani, akajitambulisha kwamba yeye alikuwa ni mke wa Jamaa niliye naye Bar akaniuliza kama kweli nipo naye nikathibitisha hilo, Hapo ndipo alipoanza kunishambulia kwamba tokea nimefahamiana na mmewe, mmewe amekuwa akichelewa kurudi nyumbani, na ameanza tabia ya Umalaya, hivyo akaniasa niache kumfundisha mmewe Tabia zangu chafu za umalaya.

Nimeumia sana kwasababu hata siku moja huwezi ukamfundisha tabia mbaya mtu mzima mwenzako, labda na yeye awe tayari anatabia hizo, huo umalaya wangu sijui kaufahamia wapi kwasababu hatujawahi kufahamiana kabla ya wao kuhamia mtaani, japokuwa wife kasafiri mda mrefu nimejitahidi sana kujizuia na haya mambo, na mbaya zaidi wife akirudi akikuta sipo katika mahusiano mazuri na Mke wa jirani ata-draw picture gani? Nifanye nini ili tuendelee kuheshimiana na huu dada? Napata taabu kwasababu nikimueleza mmewe kwamba aangalie cha kufanya ili mkewe afute imani mbaya aliyo nayo juu yangu lakini jama
-Jamii Forums
 
Support : KARIBU TENA MDADISI MAM
Copyright © 2011. RISASI - Haki Zote Zimehifadhiwa.
KWA HISANI YA MDADISI MAMBO
Proudly powered by Blogger