SIKU chache baada ya ndoa ya mastaa wawili wa filamu
Bongo, Salome Ndumbagwe Misayo ‘Thea’ na Michael Sangu ‘Mike’
kuvunjika, imedaiwa mambo ya kishirikina yanahusika kwani mauzauza
yalianza siku nyingi zilizopita.
Mtu wa karibu wa mastaa hao aliyeomba jina lake liwekwe kapuni alidai
kuwa mara kadhaa wasanii hao wamekuwa wakikumbwa na mambo ya ajabu
yaliyoashiria kuwa ndoa yao haina uhai.
“Unajua kwa nyakati tofauti pete za ndoa za Thea na Mike ziliwahi
kuwatoka kiajabu vidoleni wakiwa chooni. Haikuwa jambo la kawaida na
wenyewe walishituka na kukosa amani,” alisema mtoa habari huyo.
Hata hivyo, wahusika wamekuwa wakiamini kuvunjika kwa ndoa yao ni
mipango ya Mungu licha ya Mike kuhisi kuwepo kwa nguvu za giza katika
kuachana kwao.
“Mimi naamini kila linalotokea ni mipango ya Mungu lakini katika hili mmh, napata mashaka,” alisema Mike.
Naye The alisema: Mungu hakupanga tu tuendelee kuwa kwenye ndoa, kwa hiyo limetokea na maisha yanaendelea.”