Search in This Blog

ANGALIA FUJO ZA CHADEMA MAHAKAMANI HAPO JANA

Ni January 3 2014 asubuhi ambapo watu mbalimbali wakiwemo Wafuasi na Wanachama wa Chadema walikua wamekusanyika Mahakama kuu kanda ya 88.5 Dar es salaam wakitaka kujua kitakachotokea manake kesi ya Mbunge Zitto Kabwe dhidi ya chama chake cha Chadema ilikua inaendelea.

Muda mfupi kabla ya kuanza kusikilizwa kwa kesi hiyo, asubuhi kulitokea fujo baada ya jamaa mmoja alieshtukiwa kwamba anarekodi mazungumzo ya moja kati ya vikundi vilivyokua vimesimama kwenye kordo ya Mahakama kuanza kushambuliwa.
Yani ilikua hivi…….. wakati kesi inasubiriwa kuanza kusikilizwa kulikua na makundi mbalimbali ya hawa Wafuasi, wengine upande wa Chadema, wengine upande wa Mbunge Zitto Kabwe ambapo kwenye hivyo vikundi ndio kuna kimoja kikaanzisha vurumai baada kushtukia mchezo.
 Mpaka mwisho, hakikujulikana kilikua kikundi cha upande gani kati ya hizi pande mbili za hii kesi ambayo imeahirishwa mpaka Jumatatu January 6 2014
 
Support : KARIBU TENA MDADISI MAM
Copyright © 2011. RISASI - Haki Zote Zimehifadhiwa.
KWA HISANI YA MDADISI MAMBO
Proudly powered by Blogger