Klabu ya Bayern Munich hatimaye imethibitisha kumsajili mshambuliaji wa kimataifa wa Poland Robert Lewandowski .
Lewandowski
amesaini mkataba wa miaka mitano ambapo ataanza kuichezea Bayern Munich
mwezi julai mwaka huu baada ya kuisha kwa msimu wa sasa wa ligi ya
Ujerumani ambako atakuwa anamalizia mkataba wake na Borrusia Dortmund.
Robert
Lewandowski anatarajiwa kufanyiwa vipimo vya afya na klabu ya Bayern
Munich baada ya kusaini ikiwa ni taratibu za mwisho kabla ya kujiunga
nayo rasmi.
Lewandowski
yuko kwenye miezi sita ya mwisho ya mkataba wake na Dortmund hali
inayomruhusu kuingia makubaliano ya awali na klabu nyingine na atajiunga
na Bayern kuanzia msimu ujao ambapo anaondoka Dortmund bure.