Search in This Blog

MAMA KANUMBA ASEMA HAKUNA MSANII ANAYEMFIKIA KANUMBA HATA KWA DAWA

MAMA wa msanii aliyekuwa nguli wa filamu nchini marehemu Steven Kanumba, Flora Mtegoa  amenyanyua kinywa chake na kutema cheche kuwa katika mastaa wote wa filamu Bongo, hajaona hata mmoja wa kumfananisha na mwanaye kimuonekano na hata katika uigizaji wake.
Flora Mtegoa.
Akipiga stori na Centre Spread mama Kanumba alisema hayo kutokana na mastaa wengi kutamani awape nafasi ya kucheza kama Kanumba katika filamu yake anayoiandaa inayohusu maisha ya mwanaye tangu utotoni, na kudai katika wote hajaona mwenye kigezo cha kumpa nafasi hiyo.
http://api.ning.com/files/PITcqz*43RkKw2f5MGUiWjjeHXNgbt2HfQDbhWphHJFoE9De9lW3yfv-CdtNSPPMqcvbyM8OWSfYUGVBA-rmOwXTNUsOsl9O/KANUMBA.jpgMarehemu Steven Kanumba.
“Siyo kwamba hawana kiwango kizuri cha kumfikia mwanangu, isipokuwa kwa mtazamo wangu naona nikimshirikisha staa yoyote katika kipengele hicho nitakuwa nimevurunda kazi yangu…nitaandaa tamasha maalumu la kumsaka kijana anayefanana na Kanumba,” alisema mama huyo.
 
Support : KARIBU TENA MDADISI MAM
Copyright © 2011. RISASI - Haki Zote Zimehifadhiwa.
KWA HISANI YA MDADISI MAMBO
Proudly powered by Blogger