Ni kauli ya Waziri Mkuu Mizengo Pinda aliyoitoa bungeni alipojibu maswali ya wabunge.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda amesema si rahisi
Serikali kupiga marufuku usafiri wa pikipiki kubeba abiria maarufu kama
bodaboda licha ya kutambua kuwa ni sababu kubwa ya ajali na vifo vya
watu wengi.Badala yake, Pinda alisema kinachofanyika ni kutoa elimu kwa
kutumia vyombo mbalimbali hadi vijijini walikosambaa, kwa kuwatumia
polisi, vyuo vya Veta na asasi za kiraia ili kupunguza ajali
hizo.Kipindi cha mwaka jana pikipiki ziliua watu 771 kwa ajali 4,637
ambapo watu wengine 4,562 walijeruhiwa.
Mwaka 2011 ajali za pikipiki zilikuwa 3,326 na
kusababisha vifuo vya watu 594 na kujeruhi wengine 3,034.Pamoja na ajali
hizo, Pinda alisema Serikali inashindwa kuzisimamisha pikipiki kwa
sababu kwa upande mwingine zinasaidia.Pinda alitoa majibu hayo wakati
anajibu swali la Magdalena Sakaya (Viti maalumu-CUF) aliyetaka kujua
tamko la Serikali kuhusu usafiri huo ulioruhusiwa nchini kwa sheria ya
Bunge lakini matokeo yakawa kinyume na matarajio.
Kwa mujibu wa Sakaya, badala ya kuleta neema
iliyotarajiwa usafiri huo umegeuka balaa kwa kusababisha vifo na ulemavu
wa vijana wengi nchi nzima.Alisema waendeshaji wa pikipiki wengi
hawafuati sheria, ni wajeuri hivyo akapendekeza wapewe kozi ya miezi
mitatu ili kuwaweka sawa.