Waziri wa Nchi, Ofisi
ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi ametoa ufafanuzi
kuhusu Sh1 bilioni zilizotengwa kwa ajili ya mazishi ya viongozi wa
nchi mwaka huu, akisema ni za kununua eneo ambalo baadhi ya viongozi wa
nchi watakuwa wakizikwa.
Lukuvi alisema fedha hizo zimetengwa kwa ajili ya
kukunua eneo la hekta 129 zilizopo eneo la Iyumba mkoani Dodoma, ili
liwe linatumika kwa mazishi ya viongozi hao kwa mujibu wa Sheria ya
Maziko ya mwaka 2006.
“Fedha hizi zitalipwa kama fidia kwa wale watu wa
eneo lile, kwani tayari tulikuwa tumeshapanga kufanya hivyo,” alisema
Lukuvi na kuongeza:
“Siyo kila kiongozi atazikwa Dodoma, lakini kuna baadhi watakuwa wakizikwa eneo hilo.”
Lukuvi alisema hiyo inaonyesha kuwa nia ya Serikali kuhamia Dodoma iko palepale, ndiyo maana mwenyewe ni Mwenyekiti wa Bodi ya CDA ili kuharakisha mambo yafanyike haraka.
Lukuvi alilazimika kutoa ufafanuzi huo baada ya wabunge kulalamikia Ofisi ya Waziri Mkuu kutenga Sh1 bilioni kwa mazishi ya viongozi wa Serikali, wakati wananchi wanaishi hali duni ya umaskini.
Lukuvi alisema hiyo inaonyesha kuwa nia ya Serikali kuhamia Dodoma iko palepale, ndiyo maana mwenyewe ni Mwenyekiti wa Bodi ya CDA ili kuharakisha mambo yafanyike haraka.
Lukuvi alilazimika kutoa ufafanuzi huo baada ya wabunge kulalamikia Ofisi ya Waziri Mkuu kutenga Sh1 bilioni kwa mazishi ya viongozi wa Serikali, wakati wananchi wanaishi hali duni ya umaskini.
Lukuvi alikuwa anajibu michango ya wabunge,
akiwamo Lucy Owenya (Viti Maalumu - Chadema), aliyelalamikia kitendo
hicho akieleza kuwa haiwezekani fedha hizo zikatengwa wakati haijulikani
viongozi wangapi watakufa kwa mwaka huu.
Miongoni mwa wabunge ambao wamepinga kutengwa kwa
fedha hizo ni Mbunge wa Mwibara, Kangi Lugola ambaye alidai fedha hizo
ni ulaji kwa baadhi ya watu na kutoa wito kwa wenzake kutopitisha fedha
hizo.
Hata hivyo, tangu kupitishwa Sheria ya Maziko ya
Viongozi mwaka 2006, hakuna kiongozi ambaye amezikwa Dodoma ambako
kunaelezwa kuwa watakuwa wakizikwa. Viongozi wengi huzikwa mikoa
wanayotoka.