*********
Mahmoud Ahmad Arusha
Mtu
mmoja amefariki dunia baada ya kuvamiwa na majambazi na kupigwa risasi
ya shingoni wakati akiendesha gari kwenye maeneo ya barabara ya
Makongoro karibu na ofisi za Auwsa jijini hapa na watu watatu ambao ni
wanawake wawili na askari wa kikosi cha usalama barabarani kujeruhiwa
katika tukio hilo ambapo hadi sasa hawajatambuliwa majina.
Tukio hilo limetokea leo majira ya saa 6:30 mchana maeneo hayo wakati
majambazi hao waliokuwa kwenye usafiri wa pikipiki kulivamia gari hilo
na kupora kiasi kikubwa cha fedha majira ya saa 5 na nusu mchana na
kukimbia kusikojulikana.
Mmoja wa mashuhuda wa tukio hilo ambaye alikataa kulitaja jina lake
gazetini alisema kuwa waliona pikipiki mbili zikilifuta gari aina ya
Rav4 jekundu na baada ya kulifikia walimpiga risasi ya shingoni dereva
wa gari hilo ambapo walipolifikia kwenye gari hilo walifungua mlango na
kumtoa nje huku akitapata kabla ya kukata roho.
Alisema kuwa walipiga simu polisi walipofika hapo tukio lilikuwa
limekwisha huku majambazi hao wakiwa wameshakimbia kwa kutumia usafiri
wa piki piki mbili huku mmoja ambaye alikuwa kwenye piki piki ya pili
akiwafata wenzake mmoja alitumia kishoka kupasua kioo cha gari hilo na
kufungua mlango wa gari na kubeba begi lililokuwa na fedha na kutokomea
kusiko julikana.
Matukio ya ujambazi wa kutumia silaha mkoani hapa ambayo yalikuwa
yamekaa kimya kwa muda mrefu bila kuonekana yameonekana kuanza kujirudia
kwa kasi sasa na katika tukio hilo pia askari wa usalama bara barani
ambaye alikuwa akifuatilia Tukio hilo alipoanza kuwafuatilia majambazi
hao alivunjwa mguu kwa silaha ya moto hali ambayo ilileta taharuki kwa
wakazi wa jiji hili kwa muda.
Wakinamama hao waliotambuliwa kuwa ni wafanyabiashara walikuwa wamekodi
gari hilo wakati wakizipeleka benki ndipo walikutana na kimbembe hicho
cha uporaji wa mchana kweupe na maiti ya dereva huyo ilichukuliwa
kupelekwa kwenye chumba cha kuhifadhia maiti cha hospitali ya Mount Meru
na askari waliofika kupambana na majambazi hao.
Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo kaimu kamanda wa polisi mkoani
hapa Ibrahimu Kilongo alipotafutwa kwa njia ya simu alisema kuwa bado
wanalifuatilia tukio hilo na watatoa taarifa baadae kwa vyombo vya
habari