Search in This Blog

MSICHANA MDOGO ABAKWA INDIA

Polisi nchini India wamemkamata mwanamme mmoja kwa kuhusika na kumbaka msichana wa miaka mitano katika mji mkuu, Delhi.
Maandamano kupinga ubakaji nchini India
Msichana huyo aliumia vibaya na sasa anatibiwa hospitali akiwa mahtuti.
Mshukiwa, mwenye umri wa zaidi ya miaka 20, alikamatwa katika jimbo la Bihar zaidi ya kilomita 1000 kutoka Delhi.
Anatuhumiwa kuwa alimnyakua mtoto huyo karibu na kwao na alimzuwia kwa siku mbili.
Jumamosi maandamano kadha yalifanywa mjini Delhi.
Baadhi ya waandamanaji walieleza hasira kuhusu uhalifu huo.
Wengine waliwalaumu polisi kwa jinsi walivoshughulikia kesi hiyo.
Hilo ni tukio la karibuni kabisa katika visa kadha vya ubakaji ambavyo vimezusha hamasa nchini India.
chanzo:bbcswahili.co.uk 
 
Support : KARIBU TENA MDADISI MAM
Copyright © 2011. RISASI - Haki Zote Zimehifadhiwa.
KWA HISANI YA MDADISI MAMBO
Proudly powered by Blogger