Dar es Salaam. Benki ya Exim, imetangaza mpango wa kutoa nafasi za ajira zaidi kwa wahitimu kutoka vyuo vikuu mbalimbali nchini, ukiwa ni mpango wa benki hiyo katika kupanua ajira nchini.
Akizungumza katika maonyesho ya vyuo vikuu
yaliyofanyika katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam mwishoni mwa wiki,
Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya Exim, Dinesh Arora, alisema vyuo vikuu vina
nafasi kubwa ya kuziba pengo la upungufu wa wafanyakazi katika sekta ya
kibenki na fedha nchini.
“Baada ya kuanzishwa kwa kituo chetu cha mafunzo
kinachojulikana kama Exim Academy, benki yetu sasa imeamua kuwalenga
moja kwa moja wahitimu kutoka vyuoni, uzoefu hautakuwa kipingamizi kwa
sababu wahitimu hao watapatiwa mafunzo muhimu mara watakapojiunga na
benki yetu,” alinena mkurugenzi huyo.
“Nimebahatika kufanya usaili kwa baadhi ya
wahitimu leo (jana) na nimeona wengi wana uwezo mkubwa sana. Baada ya
zoezi hili kukamilika, tutachagua baadhi yao ili wajiunge na benki,”
alisisitiza Arora.
Meneja Mwandamizi wa Tawi la Exim la Clock Tower,
Agnes Kaganda, aliwapa changamoto wahitimu hao kuwa makini katika maisha
ili kufikia malengo na ndoto zao.
“Katika hii dunia hakuna kisichowezekana, naomba muendelee kufanya kazi yoyote itakayopatikana bila kukata tamaa na usiruhusu mtu kukuvurugia ndoto zako,” alisema.
“Katika hii dunia hakuna kisichowezekana, naomba muendelee kufanya kazi yoyote itakayopatikana bila kukata tamaa na usiruhusu mtu kukuvurugia ndoto zako,” alisema.
Kwa upande wake, Makamu wa Rais wa Kamati ya
Mandalizi ya maonyesho hayo, Wendo Lendo, alisema yametoa fursa kwa
wahitimu kujuana na kampuni mbalimbali kubwa.
Alisema maonyesho hayo yamefana sana hasa ikizingatiwa kuwa mfumo wa elimu wa Tanzania hausaidii kuwajengea wahitimu uwezo wa kuajiriwa. Zaidi ya kampuni 20 zilishiriki katika maonyesho ya mwaka huu.
Alisema maonyesho hayo yamefana sana hasa ikizingatiwa kuwa mfumo wa elimu wa Tanzania hausaidii kuwajengea wahitimu uwezo wa kuajiriwa. Zaidi ya kampuni 20 zilishiriki katika maonyesho ya mwaka huu.