Daktari katika
hospitali ya mkoa wa morogoro akiangalia mwili wa mtu anayedaiwa kuwa ni
jambazi baada ya wananchi katika kijiji cha mwanzomgumu manispaa ya morogoro kumua
huku majambazi hayo nayo yakijeruhi watu wawili na kupora kiasi cha pesa sh 2.3
mil katika soko la ndizi
kwa mujibu wa taarifa zilizotufikia
zimeeleza kuwa jumla ya majambazi watatu wenye silaha yalivamia wafanyabiashara
na wakulima na kufyatua risasi ambazo zimewajeruhi watu wawili na kulazwa
katika hospitali ya mkoa wa morogoro.
Waliojeruhi na kutambuliwa ni furaha
shomari, (30) mkazi wa mwanzo mgumu ambaye alipigwa risasi sehemu ya
ubavuni na kutokea eneo la tumbo.endelea kupitia audifacejackson blog kwa
taarifa zaidi.
mungine ni hussein ramadhan
suleiman (40) mkazi mburahani kwa jongo jijini dar es salaam ambaye naye
alipigwa risasi katika ugoko wa mguu na kudondoka chini huku mmoja wa majambazi
hao alimpola kiasi cha sh 2.3 mil pamoja na simu ya mkononi yenye thamani ya sh
80,000 katika tukio lililotokea majira ya saa 12 kasoro.
Baada ya kutokea tukio hilo
wananchi walifanikiwa kumbidhiti mmoja wao na kumshushia kipigo hadi kupoteza
maisha