Search in This Blog

MAHAKAMA YAMWACHIA HURU MSIGWA KWA DHAMANA.....


WATUHUMIWA 60 wa vurugu kati ya machinga na polisi mjini Iringa akiwemo Mbunge  wa  Jimbo  hilo, Mchungaji Peter Msigwa, kwa sasa  wanafanyiwa  utaratibu  wa  dhamana  baada ya mahakama  kukubali  kupewa  dhamana.
 
 Awali watuhumiwa  walisomewa mashitaka matatu  huku mbunge  akisomewa shitaka la  kushawishi  watuhumiwa hao kufanya  vurugu.
  
Watuhumiwa  wote  wamekana mashitaka  dhidi yao na kwa  sasa utaratibu  wa dhamana  unafanyika mbele  ya mahakama ya  hakimu mkazi  wa wilaya ya  Iringa, Mheshimiwa  Godfrey Isaya.



Mashitaka waliyosomewa watuhumiwa ni pamoja na shitaka la kwanza la mbunge ambalo ni kushawishi kufanya vurugu, huku  wengine  wote  makosa yao yakiwa ni kufanya mkutano bila kibali, kuharibu mali kinyume na sheria ni  kufanya  vurugu.
 
Support : KARIBU TENA MDADISI MAM
Copyright © 2011. RISASI - Haki Zote Zimehifadhiwa.
KWA HISANI YA MDADISI MAMBO
Proudly powered by Blogger