Khadija Shaibu ‘Dida’.
Akizungumza na paparazi mapema wiki hii katika Hospitali ya
Muhimbili, jijini Dar, Dida alisema kitendo cha kukutwa na malaria 250
katika mwili wake kilikuwa hatari sana kwani ingeweza kumuondoa uhai
kabisa.“Nilichungulia kaburi mwenzenu maana hali niliyokuwa naisikia siku ile ya kwanza ilikuwa ni nusu duniani, nusu akhera. Nilikuwa wa leo au wa kesho ila namshukuru Mungu kwa sasa naendelea vizuri,” alisema Dida.
Mwishoni mwa wiki iliyopita, Dida alipandwa na malaria kali, akakimbizwa katika Hospitali ya Amana, Ilala jijini Dar kisha kuhamishiwa Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa matibabu zaidi.