Zaidi ya watalii 1,000 na watalaam katika masuala ya matembezi ya
mbugani wameshiriki kwenye survey kubwa ya aina yake kutafuta nchi bora
zaidi kwa safari za mbugani. Matokeo yametoka na Tanzania imekuwa
mshindi.
Ngorongoro Crater
Kwa mujibu SafariBookings.com
(The largest online marketplace for African safari holidays) iliendesha
utafiti wa miaka miwili kwa kuchukua maelezo kutoka kwa waendaji wa
safari hizi mbugani pamoja na makampuni yanayojihusisha na kiwanda hicho
kuangalia ni nchi ipi bora zaidi barani Afrika.
Ikipata nyota 4.8 kati ya nyota 5, Tanzania imeibuka mshindi kwa
kuizidi Botswana kwa takriban point 10. Nchi zingine zilizoingia fainali
ni pamoja na Kenya, Zambia na Afrika Kusini.
Utafiti huo ulijikita kupitia michanganuo 2,305 kutoka watembeaji
wenyewe na 756 kutoka kwa wataalam kwenye industry hiyo yenye watalii
wengi miongoni mwao wakiwemo waandishi wa mitandao/vitabu kuhusu masuala
hayo ikiwemo Lonely Planet, Rough Guides, Frommer’s, Bradt na
Footprint.
Sababu kubwa Tanzania imechaguliwa kama nchi bora ni kwasababu ni
maskani pa maeneo mawili maarufu kwa watalii duniani, mbuga ya wanyama
Serengeti na Ngorongoro Crater.
Sehemu zote mbili hutoa muonekano wa kuvutia za maisha halisi ya porini kuonekana duniani.
Flamingo wa Ziwa Manyara
Pamoja na Serengeti na Ngorongoro zilizopo kaskazini mwa Tanzania,
maeneo ya Magharibi na Kusini yana vivutio vingine muhimu kama hifadhi
za taifa za wanyama za Gombe na Mahale huku hifadhi ya Katavi
ikijulikana kwa wingi wake wa vifaru na nyati.