Wakazi wa mji wa Rjukan nchini Norway
ni kati ya watu ambao wanategemea kupata jua la masika kwa mara ya
kwanza katika kipindi cha masika, baada ya mji huo kutopata jua la moja
kwa moja kwa miaka 100 sasa katika kipindi hicho.
Ili kuondokana na giza na baridi katika kipindi cha msimu wa ‘winter’
halmashauri ya mji huo imetumia zaidi ya pesa ya Norway kronor milioni 5
(zaidi ya billioni 1) kuweka vioo tatu vikubwa ‘heliostats’
vilivyotegeshwa juu ya bonde ikiwa ni mita 450 juu ya mji
vitakavyomulika jua halisi na kumulika katika mji huo.
Helikopta zitatumika kufunga vioo hivyo na zitakuwa zikifuatilia
mwenendo wa jua na kumulika mwanga moja kwa moja katika ‘main square’ ya
mji wa Rjukan ili kuwasaidia wakazi wa mji huo mdogo ambao wamekuwa
wakifunga safari kila mwaka kwenda juu ya mlima mrefu ili kupata joto
la jua halisi.