Search in This Blog

WANAFUNZI 58 WANUSURIKA KIFO MKOANI MARA

 Wanafunzi 58 wa shule ya sekondari ya Mmazami wilayani butiama mkoani  Mara, wamelazazwa katika hospitali za  Butiama na ya mkoa wa Mara mjini Musoma baada ya kupata ajali mbaya kufuatia gari walikuwa wakisafiria kutoka shuleni hapo kwenda  shule ya sekondari ya Butuguri kwa shughuli za michezo kupinduka.
Majeruhi hao ni miongoni mwa wanafunzi 136 walikuwa wakisafiri kutumia gari aina ya  fuso yenye namba za usajili T 737 AHR, ambayo inadaiwa kupinduka ndani ya kijiji cha  Butuguri baada ya dereva wake Bw Francis Marwa kushindwa kuimudu kono mbaya ambayo iko katika barabara hiyo.
Daktari wa zamu wa hospitali ya butiama Dk. Gitera Nyange, amesema hospitali yake  imepokea majeruhi 40 na wengine 18 kupelekwa hospitali ya mkoa na kati ya hao  watatu walikuwa katika hali mbaya lakini madakatari wameweza kuokoa maisha ingawa  mmoja walilazimika pia kupeleka hospitali ya musoma baada ya kugundua kuwa  amevunjika paja la mguu wake wa kulia.
Kwa upande wake mwenyekiti wa halmashauri ya butiama Bw Magina Magesa ambaye  ametembelea majeruhi hao katika hospitali hizo kwajili ya kutoa pole kwa wanafunzi  hao, amesema ingawa wanafunzi wengi wanaendelea vizuri lakini madaktari  wameombwa kufanya uchunguzi wa kina na kuona wale wanahitaji kupelekwa hospitali ya rufaa ya Bugango jijini Mwanza wapelekwe mara moja.


 
Support : KARIBU TENA MDADISI MAM
Copyright © 2011. RISASI - Haki Zote Zimehifadhiwa.
KWA HISANI YA MDADISI MAMBO
Proudly powered by Blogger