STAA wa sinema za Kibongo, Skyner Ally ‘Skaina’ amepotea kwenye gemu
chanzo kikidaiwa kuwa ni mapenzi kwani kila mwanaume anayeanzisha naye
uhusiano wa kimapenzi, humzuia kuendelea kufanya kazi za sanaa.
‘Akibadilishana
sentensi’ na mwandishi wetu, rafiki wa karibu wa msanii huyo ambaye
hakupenda jina lake liandikwe gazetini, alisema kitendo cha wanaume
wengi wanaoanzisha uhusiano na Skaina kumzuia kuendelea na kazi ya
uigizaji, kimechangia kumpoteza.
Mwandishi wetu ‘alipomvutia waya’ Skaina, aliambulia majibu ya ‘sintofahamu’ huku akisisitiza kutosumbuliwa.
“Sasa
kama umeambiwa hivyo mnachoniuliza hapo ni nini? Kwani lazima niigize
mara kwa mara? Mimi naipenda kazi yangu, sitaki maswali zaidi,” alisema
Skaina.