Mashuhuda wa tukio hilo ambao ni wakulima
walidai kuwa walikuta mwili wa mwanamke huyo ukiwa uchi huku mikono yake ikiwa
imefungwa kwa kutumia ribbon,koo lake na pua yake vilikuwa vimekatwa kwa
kutumia kitu chenye ncha kali.Pia mwili huo ulikutwa ukiwa na jeraha begani.
Wakisimulia tukio hilo wakulima hao walidai
nguo za maiti huyo zilikuwa zimetupwa mita 1 kutoka eneo la tukio.
Baada ya kufanyika uchunguzi ndipo ilipo
bainika kuwa mwanamke huyo ambae alitambuliwa kwa jina moja tu la victoria
mwenye umri wa miaka 33 ni mkazi wa kijiji cha San Nicolás Tetelco.
Mamlaka husika ilidai kuwa
kabla ya kuuawa victoria alibakwa na mtu aliye mbaka ni mwanakijiji mwenzake
ambae aliamua kumuua akihofia kama angemuacha marehemu basi yeye ange kamatwa
kutokana kitendo hicho cha kinyama