Search in This Blog

MTUHUMIWA WA USHIRIKINA AUWAWA KWA MAPANGA

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi, Dhahiri Kidavashari
Kamanda wa polisi mkoa wa Kitavi
MKAZI wa Kijiji cha Kapalala Tarafa ya Nsimbo Wilaya ya Mlele Mkoa wa Katavi , Mele Seni (60) ameuawa kikatili kwa kukatwa mapanga kichwani na mgongoni na watu wasiofahamika wakati akiwa nyumbani kwake akiota moto, sababu kubwa ikielezwa kuwa mzee huyo alikuwa anatuhumiwa kwa ushirikina.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi Dhahiri Kidavashari alithibitisha kutokea kwa tukio hilo lililotokea jana saa moja na nusu usiku wakati Seni akiwa anaota moto nyumbani kijijini hapo.

Alisema siku hiyo ya tukio Seni akiwa nyumbani kwake amejipumzisha akiota moto ghafla walitokea watu wasiofahamika na kupiga hodi nyumbani kwa Seni ambapo aliwakaribisha akidhani ni watu wema.

Inadaiwa ndipo watu hao wakiwa na mapanga walipoanza kumshambulia Seni kwa kumkata kwa panga kwenye kichwa na mgongoni huku akipiga mayowe kuomba msaada kwa majirani zake.
 
Support : KARIBU TENA MDADISI MAM
Copyright © 2011. RISASI - Haki Zote Zimehifadhiwa.
KWA HISANI YA MDADISI MAMBO
Proudly powered by Blogger