Search in This Blog

TIBA ZA NYOKA, KONOKONO ZANAWIRI ULAYA


Nyoka wakiutambaa mwili wa binadamu, utafiti umebaini kuwa tiza za nyoka zimeendelea kushamiri sana katika bara la Ulaya na Asia. Picha na Maktaba 
Wakati nyoka akiendelea kuwa adui mkubwa wa binadamu na konokono kuonekana mdudu anayetia kinyaa kwa baadhi ya watu, nchi za China na Japan wanyama hawa wamekuwa wakitumika kama mboga na wakati mwingine wamekuwa ni rafiki wa binadamu kwani wengi wao hufugwa na binadamu.
Lakini Ukistaajabu ya Musa utayaona ya Firauni, kwani katika nchi za Ulaya miezi kadhaa iliyopita watu mbalimbali wameanza kupokea tiba kutoka kwa wanyama hao ikiwemo huduma ya kukanda na kupodoa uso (facial) inayotolewa na konokono na kusinga (massage) inayotolewa na nyoka.
Facial ya konokono
Kwa wengi wetu konokono ni mdudu mpole zaidi kuliko wadudu wengine wanaopatikana majanini, lakini nchini Japan wataalamu wamegundua kuwa lami (uteute) anaotoa mdudu huyo ni tiba nzuri kwa ngozi ya binadamu, baada ya kutumika kwa miezi kadhaa nchini Japan sasa tiba hiyo imeanza kupendwa barani Ulaya, kama watu wanavyomiminika katika saluni moja iliyopo East Midland nchini Uingereza.
Matibabu hayo yanahusisha konokono kuanzia watatu ambao huwekwa juu ya uso wa binadamu na wao huanza kuzunguka maeneo mbalimbali ya uso huo, yamekuwa yakiongeza uwingi wa watu katika saluni za maeneo mbalimbali ya nchi za Ulaya.
Wataalamu hao wa facial ya konokono akiwamo Dk Sunil Chopra wanasema kwamba katika matibabu hayo huwa wanahakikisha kwamba konokono anatembelea kila sehemu ya uso wa binadamu isipokuwa maeneo ya mdomo, macho na pua.
Kwa mujibu wa mmiliki wa Simply Divene Saloon iliyopo Corby katika mji wa Northamptonshire nchini Uingereza, Diane Gower matokeo ya tiba hiyo inayogharimu kiasi cha dola 50 sawa na Sh80,000, huonekana papohapo na kwamba wadudu hao hutoa kamasi zenye protini muhimu kwa ngozi ya binadamu.
Anasema, “Mwanzoni kwa mteja wa kwanza huwa wanashtuka sana kwani anapokutembea usoni huona kuwepo kwa hali isiyokuwa ya kawaida, lakini wateja wetu huhisi raha ya ajabu pindi konokono wanapoendelea kutambaa kwenye nyuso zao kwa matibabu.”
Facial ya konokono ilianzishwa katika saluni iitwayo Tokyo’s Clinical Saloon nchini Japan na mtu wa kwanza kupatiwa huduma hiyo alikuwa ni mtu mmoja maarufu nchini humo, Escargot Course mwanzoni mwa msimu huu na kulipia gharama ya dola 161 sawa na Sh 257,600.
Konokono 60 wanamilikiwa na Gower na wamekuwa wakipewa vyakula maalumu, ikiwemo matunda na mboga za majani.
“Hivi sasa watu wengi nchini Japan wanazalisha konokono kwa ajili yetu na hata wengine wanazalisha kwa ajili ya chakula kama utamaduni wetu ulivyo lakini wanatofautiana,” alisema Gower na kuongeza; “Hii si aina ambayo unaweza ukaipata katika bustani, tumekuwa tukiwaelekeza tunahitaji wa aina gani, hata hivyo tunawapa majina ya aina ya konokono tunaowahitaji pia.”
Anasema wafanyakazi wote wa saluni wamepewa mafunzo maalumu ya kushika konokono wanapomhudumia mteja, wengine wanajifunzia katika saluni hiyo na baadaye wanakwenda kufanya kazi sehemu nyingine tofauti.
 
Support : KARIBU TENA MDADISI MAM
Copyright © 2011. RISASI - Haki Zote Zimehifadhiwa.
KWA HISANI YA MDADISI MAMBO
Proudly powered by Blogger