Mike Sangu na Ndumbagwe Misayo ‘Thea’ siku ya ndoa yao.
Ndoa
ya mastaa wa filamu, Mike Sangu na Ndumbagwe Misayo ‘Thea’ imevurugika
baada ya kutokea hali ya kuzinguana kwa wawili hao chanzo kikidaiwa ni
kukosekana uaminifu.
Chanzo cha
habari hii ambacho ni rafiki wa Thea kilieleza kuwa, kutibuana kwa
wanandoa hao kumekua kufuatia Thea kuhisi mwenzake anamzunguka.“Kimsingi
hali si shwari, ndoa inawaka moto, Thea anamtuhumu Mike kuwa
anamsaliti, chanzo ni hizi simu na siku hiyo mtiti ulipotokea, shosti
alikwenda kwao na mpaka leo hii (Juzi Jumatato) anasubiri wasuluhishwe,”
kilidai chanzo hicho.
Baada ya kupata taarifa hizo, Mike alitafutwa na alipoulizwa kuhusu ndoa yake kutibuka alisema: “Mh! Watu ni wambeya sana mimi na mke wangu tulitokea kutoelewana na si mambo ya meseji wala wanawake, mimi sina mambo hayo kabisa, siwezi kuongelea mambo mengi mpaka nitakapoenda nyumbani kwa mke wangu lakini kilichotokea ni cha kawaida tu .”Thea hakuweza kupatika kuzungumzia ishu hiyo.
Baada ya kupata taarifa hizo, Mike alitafutwa na alipoulizwa kuhusu ndoa yake kutibuka alisema: “Mh! Watu ni wambeya sana mimi na mke wangu tulitokea kutoelewana na si mambo ya meseji wala wanawake, mimi sina mambo hayo kabisa, siwezi kuongelea mambo mengi mpaka nitakapoenda nyumbani kwa mke wangu lakini kilichotokea ni cha kawaida tu .”Thea hakuweza kupatika kuzungumzia ishu hiyo.