Search in This Blog

JOHARI ASEMA MAPENZI KUWA SUMU YA MAISHA, HII NI BAADA YA KUTOSWA NA RAY

SIKU chache baada ya kuingia katika mgogoro na msanii mwenzake, Chuchu Hans kwa madai ya kugombea penzi la Vincent Kigosi ‘Ray’, muigizaji Blandina Chagula ‘Johari’ amesema amegundua mapenzi yanaumiza na ni sumu mbaya maishani.
Blandina Chagula ‘Johari’.
Akizungumza na mwandishi wetu mwishoni mwa wiki iliyopita katika moja ya mahojiano maalumu, Johari alisema mapenzi si kitu cha kuendekeza kwani ni hatari na ndiyo maana baadhi ya watu hufikia hatua ya kuchukua uamuzi mgumu wa kujiua.
“Mapenzi ni kitu kingine kabisa, sikuwahi kujua ni kwa nini baadhi ya watu hufikia hatua ya kukatisha maisha yao kisa mapenzi, hakika mapenzi ni sumu kali sana maishani usipojiongoza,” alisema Johari.
 
Support : KARIBU TENA MDADISI MAM
Copyright © 2011. RISASI - Haki Zote Zimehifadhiwa.
KWA HISANI YA MDADISI MAMBO
Proudly powered by Blogger