Timu ya taifa ya Tanzania Bara
‘Kilimanjaro Stars’ imeshika nafasi ya nne michuano ya Kombe la CECAFA
2013 inayofanyika nchini Kenya baada ya kufungwa na timu ya Zambia kwa
penalti 6-5.
Mchezo huo uliokuwa wa kutafuta mshindi
wa tatu wa kombe hilo ulikuwa na ushindani mkubwa ambapo bao la Zambia
lilifungwa na Ronald Kampamba katika dakika ya 51 na Kilimanjaro Stars
ilisawazisha kupitia kwa Mbwana Samatta katika dakika ya 65 kipindi cha
pili ambapo dakika 90 ziliisha kwa sare ya bao 1-1.
Wachezaji wa Kilimanjaro Stars waliopata
penalti ni Mbwana Samatta, Erasto Nyoni, Himid Mao, Amri Kiemba na
Ramadhan Singano ‘Messi na waliokosa ni Haruna Chanongo, Mrisho Ngassa
na Kelvin Yondani.