Manchester
United imeendelea kuwa na msimu mbaya baada ya kupigwa bao 1-0 katika
mechi iliyomalizika muda mfupi uliopita kwenye Uwanja wa Old Trafford
wakati ilipokuwa ikipambana na Newcastle United katika mchezo wa
Premier.
Kipingo hicho ambacho ni cha tano kimeifanya Man United iwe
na msimu mbaya kuliko yote ndani ya kipindi cha miaka 20 iliyopita,
ambapo Jumatano iliyopita, United ilifungwa bao 1-0 na Everton katika
ligi hiyo.
Bao la Newcastle lilifungwa na Yohan Cabaye katika dakika ya 61.