Search in This Blog

DUBAI YAWEKA REKODI YA DUNIA KATIKA KUSHEREHEKEA MWAKA 2014, ONA VIDEO YAKE JINSI WALIVYOSHEREHEKEA

Fataki zipatazo 500,000 zenye rangi tofauti tofauti kwaajili ya kuupokea mwaka mpya 2014 ziliandaliwa kwa takriban miezi mitano, mtandao wa Guinness World Records umeripoti.
Fataki hizo zilidumu kwa dakika sita kuanzia saa 6 kamili usiku wa 01/01/2014.
Dubai Jengo la Burj Khalifa Dubai wakati wa mchana
Waandaaji wa fataki hizo walilenga kuvunja rekodi iliyowekwa mwaka 2012 katika Golden Jubilee Anniversary ya Kuwait.
Fataki dubai-2
Jumla ya computer 100 zilitumika kuleta muonekano wa fataki hizo za Dubai zilizoambatana na muziki uliotengenezwa maalum kwaajili ya shughuli hiyo (choreographed musical soundtrack).
Rais wa Guinness World Records Alistair Richards aliyesafiri kutoka Uingereza hadi Dubai maalum kwaajili ya kushuhudia fataki hizo wakati wa kuupokea mwaka mpya alisema, “The scale of this record attempt is truly impressive and will ensure all eyes are on Dubai”.
Tazama video ya fataki hizo
 
Support : KARIBU TENA MDADISI MAM
Copyright © 2011. RISASI - Haki Zote Zimehifadhiwa.
KWA HISANI YA MDADISI MAMBO
Proudly powered by Blogger