Kocha wa Man United, David Moyes
KLABU ya Manchester United inahofia
jitihada zake za beki mpya wa kushoto katika usajili wa dirisha dogo Januari
hauwezi kuvunja matunda, kwa Everton na Southampton kutokuwa na mpango wa
kuwaachia wachezaji wake Leighton Baines na Luke Shaw.
Kocha wa United, David Moyes
alijaribu bila mafanikio kutaka kumsaini Baines kutoka klabu yake ya zamani mapema
msimu huu, baada ya Patrice Evra kusema anahitaji ushindani wa maana wa namba
katika nafasi yake.
Lakini juhudi za United zimezimwa na
Mwenyekiti wa Everton, Bill Kenwright na pamoja na hayo Moyes ameambiwa na
Mtendaji Mkuu wa klabu yake, Ed Woodward kwamba hana fedha za kutoa kwa ajili
ya usajili wa mwezi ujao.
Mabingwa hao wa Ligi Kuu ya England
wanahofia watakutana na mazingira yale yale kutoka klabu ya Merseyside, pamoja
na Southampton juu ya Shaw wanayemtaka.
Shaw, mwenye umri wa miaka 18, pia
yupo kwenye rada za Chelsea, lakini Southampton imeweka wazi kwamba haimuuzi
mchezaji huyo.
United inahaha kusaka beki wa kushoto
kutokana pia na Mholanzi, Alexander Buttner kushindwa kufanya vizuri tangu
asajiliwe na Sir Alex Ferguson mwaka 2012.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka
24, binafsi anatakiwa na Tottenham katika usajili huu wa Januari, ameanza
katika mchezo mmoja tu wa Ligi Kuu msimu huu, maana yake kwamba Evra, akiwa na
umri wa miaka 32, amebeba majukumu makubwa ya timu katika nafasi hiyo.
Tayari msimu huu, beki huyo wa
Ufaransa amecheza mechi 29 za klabu yake na hi yake katika mashindano yote.
Chanzo: binzubeiry
A