Rais Jakaya Kikwete.
Rais Kikwete akiambatana na Mama Salma Kikwete na ujumbe wake, waliondoka nchini jana mchana kwenda Uholanzi tayari kwa ziara hiyo ambako pia ataandamana na Mawaziri wanne wa Serikali.
Mawaziri hao ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe, Waziri wa Viwanda na Biashara, Dk. Abdallah Kigoda, Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo na Waziri wa Maji, Ardhi, Nishati na Maendeleo ya Makazi wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Ramadhan Shaaban.
Leo Rais Kikwete atafanya mazungumzo rasmi ya Kiserikali kati ya Tanzania na Uholanzi kwenye Makazi Rasmi ya Waziri Mkuu. Mazungumzo hayo rasmi yatakuwa kati ya Rais Kikwete na ujumbe wake na Waziri wa Mambo ya Nje wa Uholanzi, Frans Timmermans.
No comments:
Post a Comment