Search in This Blog

BAYERN MUNICH YAILAZA FC BARCELONA 2-0.

On target: Philip Lahm (centre) struck early on for Bayern Munich as the Germans took controlKama kawaida: Philip Lahm (katikati) akishangilia na wenzake baada ya kufunga bao la mapema
Good going: Pep Guardiola's side looked strong and imposing against BarcelonaMwendo mzuri: Kikosi cha Pep Guardiola  kimeonekana kuwa imara zaidi na kuwatwanga Barcelona
Woe: It was a disappointing first half for Barcelona captain Messi and then he was substitutedHovyo kweli: Nahodha wa Barca, Lionel Messi alicheza vibaya katika kipindi cha kwanza na kutolewa
Double up: Mario Mandzukic scored the second from close range to seal the gameChuma cha pili: Mario Mandzukic akifunga bao la kuwazamisha wanaume wa Katalunya 
Opener: Lahm celebrates after heading past Pinto to give Bayern a 1-0 leadUfunguzi wa mabao: Lahm akishangilia baada ya kuifungia klabu yake na kuongoza kwa  1-0 
Edging through: Thiago (left) and Boateng (right) challenge Messi for the ballKazi na dawa: Thiago (kushoto)na Boateng (kulia) wakimghasi  MessiFight for the ball: Frank Ribery of Muenchen challenges Marc Bartra Vita ya kuwania gozi: Frank Ribery wa Bayern akiwania mpira na Marc Bartra wa Barca.
Strolling: Guardiola seems to have it easy with Bayern, given their strong squad and winning waysImara kama kawaida: Guardiola anaonekana kuwa na kazi nyepesi na Bayern yake, wametumia kikosi cha moto kuwashinda Barca 
Blowing one's trumpet: Musicians in traditional costumes perform in the stadium before the gameBurudani kama kawaida: Wanamuziki wa asili wakivalia kitamaduni wakitumbuiza kabla ya mchezo kuanza
Star attraction: Messi started for Barcelona in the Allianz ArenaKivutio cha wengi: Messi alianza katika kikosi cha kwanza cha Barcelona, Allianz Arena.

Na Baraka Mpenja kwa msaada wa Sportsmail.com
Kocha wa wekundu wa kusini mwa Ujerumani, “Bavarians” Bayern Munich, Joseph  Pep Guardiola ameifunga klabu yake ya zamani ya FC Barcelona mabao 2-0 katika mechi ya kirafiki  uwanja wa Allianz Arena jijini Munich nchini Ujerumani .

Nahodha  Philipp Lahm alifungua bao la kwanza dakika ya 14, lakini hadi dakika 45 za kipindi cha kwanza zinamalizika, Bayern walikuwa mbele kwa bao moja. Bao la pili lilifungwa na Mario Mandzukic katika dakika ya  87 na kipute hicho kumalizika kwa ushindi kwa Bayern ambao wanaonekana kuwa na morali kubwa ya kufanya makubwa msimu wa 2013/2014.
 
Japokuwa Bayern wamepata wamesubiri mpaka dakika za lala salama kutia kambani bao la pili, lakini walifanya kazi nzuri ndani ya dakika zote 90 na hii inadhihirisga kwamba msimu ujao utakuwa mzuri kwao, hivyo wapinzani wao wa barani Ulaya wanatakiwa kuchukua tahadhari kubwa.

Kikosi cha Bayern Munich: Neuer (Starke 46), Rafinha, Dante (Van Buyten 59), Boateng, Alaba, Thiago, Lahm (Gustavo 59), Kroos, Ribery, Robben (Shaqiri 46), Muller (Mandzukic 46).

Mabaol: Lahm 14, Mandzukic 87. Kikosi cha Barcelona: Pinto (Oier 46), Montoya (Kiko 46), Bartra (Gomez 46), Mascherano (Planas 46), Adriano (Patric 46), Song (Espinosa 46), Sergi Roberto (Ilie 46), Dos Santos (Quintilla 46), Tello (Joan Roman 46), Messi (Dongou 46), Alexis (Dani Nieto 46

Bayern walitawala sana mchezo huo na huenda wangepata mabao mengi zaidi kama safu yao ya ushambuliaji ingetulia kubadili nafasi walizopata kuwa mabao.
 
Support : KARIBU TENA MDADISI MAM
Copyright © 2011. RISASI - Haki Zote Zimehifadhiwa.
KWA HISANI YA MDADISI MAMBO
Proudly powered by Blogger