Search in This Blog

BARNABAS NA SHILOLE WASHINDAANA, LAKINI MPAKA SASA MCHEZO UPO DROO, KWANI KILI MMOJA AMEVUTA NDINGA LA MIL 25

FEDHA inaongea. Siku chache baada ya mwanamuziki Zuwena Mohamed ‘Shilole’ kuvuta mkoko Toyota Lexus, mkali wa Bongo Fleva, Elias Barnaba naye amemjibu kwa kuvuta Mark X.
                             Mkoko mpya wa mwanamuziki Zuwena Mohamed ‘Shilole’ aina ya Toyota Lexux.
Barnaba ambaye aliwahi kuwa na uhusiano wa kimapenzi na mwanamuziki huyo kisha wakamwagana, ameamua kuvuta gari hilo ambalo lina thamani ya Sh. Mil 25 sawa na lile la Shilole.
Akizungumza na paparazi wetu, Barnaba aliweka plain kuwa amenunua mkoko huo ambao anaamini utaendana na mishemishe zake za kimuziki ambapo kwa wakati huu ameona gari hilo ndilo linamfaa.
                                                     Elias Barnaba naye amemjibu kwa kuvuta Mark X.
“Namshukuru Mungu kwamba ndoto zangu za kuvuta gari ya aina hii zimetimia, sijui huko mbeleni nitakuwa na ndoto za kumiliki gari gani lakini kwa sasa acha nikae humu kwanza,” alisema Barnaba.
Kabla ya kununua mkoko huo, Barnaba staa wa songi la Sorry alikuwa akimiliki gari aina ya Oppah yenye thamani ya Sh. Mil 16 sawa na Shilolo ambaye pia alikuwa na gari aina hiyo kabla ya kununua Toyota Lexus.
JIUNGE NA UKURASA WETU WA FACEBOOK KUPITIA HAPA >>MDADISI MAMBO
 
Support : KARIBU TENA MDADISI MAM
Copyright © 2011. RISASI - Haki Zote Zimehifadhiwa.
KWA HISANI YA MDADISI MAMBO
Proudly powered by Blogger